skip to Main Content
+255754 354681 info@hakielimu.or.tz

Uzinduzi wa ripoti ya utafiti wa Mchango wa Elimu ya Uraia Shule za Sekondari na Ushiriki wa Vijana Katika Mchakato wa Kidemokrasia

Utafiti uliofanywa na asasi ya kiraia ya HakiElimu umeonesha kuwa sehemu kubwa ya walimu ambao wanafundisha somo la uraia hawana maarifa stahiki yanayowawezesha kuwafundisha na kuwaaandaa vijana ngazi ya sekondari katika kuelewa maana ya siasa safi na umuhimu wa ushiriki wao katika mifumo ya kidemokrasia katika ngazi ya shule, familia na jamii. 

Hali hii ni kinyume na matarajio ya wanafunzi hawa ambao kwa upande utafiti huu umeonesha kuwa wanategemea shule kama njia kuu ya kujifunza na kujengewa uzoefu katika michakato ya kidemokrasia ukilinganisha na vyanzo vingine mfano radio, televisheni, magazeti, mitandao ya kijamii na kujisomea vitabuni. 

Utafiti huo pia umeonesha kuwa somo la uraia halichukuliwi kuwa ni la umuhimu na lazima shuleni kwa sababu Mwalimu yoyote anaweza kufundisha somo hili pasi kulisomea na pia limetengewa muda mchache wa kujifunza kama ilivyo kwa masomo ya hiyari ya muziki na dini.

Back To Top